Sunday, April 10, 2016

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko


Matikiti maji aina ya  Sugar baby inachukua siku 60 tu kuvuna ukiongeza na  siku 3-5 za kukaa ardhini, zao hili unaweza kulima mara  4  mwaka. Mfano ukiwa na  ekari 5  kila eka moja inaweza kukuingizia Milioni 2 hadi 3.

Mambo muhimu
  • Nafasi inayotakiwa  ni 2mm toka mmea mmoja kwenda mwingine
  • Kila shimo unaweza weka mbegu 2 ambazo zinazaa matunda 2 hadi 3 
  • Kila shimo unaweza kupata matunda 4 hadi 6 ( wastani matunda 5).
  • Kwa ukubwa  wa ekari 5 unaweza kuwa na mashimo 1000 hadi 1200
  • Idadi ya matunda: Mashimo x Matunda kwa shimo x ekari (1,000 x 5 x 5 = 25,000)
Mapato: wastani wa shilingi 500 kwa tikiti x idadi ya matikiti kwa eneo la ekari 5 (25,000 x 500 = 12,500,000)
Mapato kwa mwaka: 12,500,000 x 4= 50,000,000
Gharama za uendeshaji wa shamba ni Tsh 25,000,000
Faida Kuu ni Tshs 25,000,000 Milioni.

1 comment:

  1. am jovin ntamamilo from university of dar es salaam
    je naomba kuuliza ni sehemu gani matikitiki maji yanamea na kuzaa vizuri

    ReplyDelete